Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kulia), Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi Jame...
Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kulia), Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi James Mbatia (katikati) na Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba.
Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) umesema umemkaribisha rasmi Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Lowassa kujiunga nao katika harakati za kuking’oa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Mbatia: Tunamkaribisha rasmi aliyekuwa waziri mkuu mstaafu, Edward Ngoyaye Lowasa kujiunga na UKAWA, ni mchapakazi makini na mtekelezaji wa majukumu, UKAWA ndio tumaini la Tanzania, tusikubali kunyamaza pale ambapo sauti zetu zinazimwa kwa lazima. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki UKAWA, UKAWA ndio tumaini letu.
Waziri mkuu mstaafu, Edward Ngoyaye Lowasa.
Mbatia: Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu, kila chama kilichosajiliwa ni mpinzani kwa mwenzake. Watanzania wanahitaji kutengenezewa katiba ambayo itaweka mfumo safi. Mwanzoni wa mwezi wa nane(wiki ijayo) tutamtangaza mgombea wetu kwa mbwembwe, tumeshapiga hatua ambayo ni nzuri
Lipumba: “Lowasa alishasema yeyote mwenye ushahidi aulete..hapa tumekaribisha Watanzania wote kujiunga.
Kuhusu CUF kusuasua UKAWA: Chama chetu hakijasusua bali kilikuwa kinafuata taratibu za chama na mkutano mkuu umebariki, yeyote atakaechaguliwa kupitia UKAWA, mimi nitamuunga mkono, chama kimebariki maamuzi haya, unapozungumza na mwenyekiti wa CUF basi ndio unazungumza na CUF.
COMMENTS