MBATIA AJIBU HOTUBA YA DR. SLAA LEO

Mwenyekiti mwenza wa UKAWA James Mbatia ameongea mchana huu na waandishi wa habari na kujibu baadhi ya mambo aliyosema Dr. Slaa hivi ndiv...

East Africa Television (EATV)'s photo.
Mwenyekiti mwenza wa UKAWA James Mbatia ameongea mchana huu na waandishi wa habari na kujibu baadhi ya mambo aliyosema Dr. Slaa
hivi ndivya alivyo ongea MBATIA
Mbatia: Napenda kuwaomba Watanzania tusimame wote kupata Katiba mpya ambayo ndiyo ajenda ya mgombea wetu Lowassa.
Mbatia: Watanzania naomba waelewe UKAWA tunasimamia utu, uzalendo, uadilifu, umoja, uwazi, uwajibikaji ndani ya Tanzania.
Mbatia: Wanasiasa hasa wale wa CCM Mwakyembe na Sita, wanaotaka midahalo waje waongee na mimi wasimsumbue Mgombea wetu Lowassa sio saizi yao.
Mbatia: Hivi ni ashiria kwamba CCM wameshindwa hoja, mara kuleta mambo ya udini, mara wanaibua hili mara lile. wanataka kuchafua amani yetu kwa kuigiza masuala ya dini
Mbatia: Wagombea wetu urais walikaa na Dokta Slaa alisema mimi ni bora kuliko wote,leo hii anasema hajawahi kutia nia,kweli?
Mbatia: Tukisema tuibue masuala yote na kashifa za kuuzwa kwa nyumba, kuna mtu atabaki salama?
Mbatia: Eti Lowassa akija ndani ya Ukawa atakuja na Wenyeviti wa CCM..hakuwahi kusema..kayasemea wapi?
Mbatia: Wewe unasema ni muadilifu ulipewa Milioni 500 mwaka 2008 unakuja kusema leo baada ya miaka 7? Tuwe wakweli.
Mbatia: Eti suala la rushwa zaidi ya miaka 7 usiripoti halafu uje useme leo, kusema uongo ni kazi sana.
Mbatia: Napenda kuwaomba watanzania wote ambao ni zaidi ya milioni 46, wasiruhusu nchi yetu ikaharibiwa na watu 100.
Mbatia: Wakenya walisema hata kama ana makosa, walisema huyo huyo tunamtaka, wakampigia kura na leo ni Rais wao.
Mbatia: Watu wachache wanaotaka eti kwa lolote lile lazima waendelee kubaki madarakani, tunasema hapana.
Mbatia: Lazima tufute mfumo huu uondoke tuwe na Tanzania mpya.
Mbatia: Napenda kuwaomba wale Viongozi wa dini walionewa kwa yale ya jana, wasamehe na waachane nayo.
Mbatia: Lowassa hajawahi kutamka kuwa nikija ndani ya UKAWA nitakuja na wabunge 50, wenyeviti wa CCM na Makatibu nk.
Mbatia: Kama hana faida haya mafuriko tungepata wapi? Nyota ya Lowassa inang'aa hata wafanye nini hawamuwezi huyu jamaa
Mbatia: Hatuna haja ya kuanza kumjadili, hiyo ni kulipasua Taifa la Tanzania kwa maslahi binafsi
Mbatia: Kilichotusikitisha ni yeye kuhusisha watu wengine wasiohusika kwenye jamii yetu, viongozi wa dini wenye heshima zao, acha sisi vyama vya siasa tusuguane wenyewe.
Mbatia: Zimebaki siku 50 na kitu, haki itendeki na nchi yetu ibaki na amani siku zote
Mbatia: Anasema kaja kupambana na Lowassa kwakuwa anagombea urais, sasa Sumaye naye anagombea urais?
Mbatia: Nimesoma barua ya ufisadi, ufisadi ni mfumo na Lowassa wana haki ya kujielezea zaidi wakitaka lakini hawa wanataka kututoa kwenye reli tuanze kujibizana mmoja na wengine.

(source eatv)

COMMENTS

Name

AJIRA AND SCHOLARSHIPS,3,CELLEBS,5,love tips,1,MAGAZETI,5,michezo,8,MIX-NEWS,11,New audio,36,politics,1,sports,4,stori za mapenzi,1,technology,1,video,28,
ltr
item
MSABAHA BLOG: MBATIA AJIBU HOTUBA YA DR. SLAA LEO
MBATIA AJIBU HOTUBA YA DR. SLAA LEO
https://fbcdn-photos-e-a.akamaihd.net/hphotos-ak-xpt1/v/t1.0-0/s480x480/10645163_1306947535986328_2550566020524929463_n.jpg?oh=8c182b60bb04c9822bd1722298c85e7e&oe=56801AF9&__gda__=1450499061_0591b4719ab321f3286d4037126f9590
MSABAHA BLOG
http://msabaha.blogspot.com/2015/09/mbatia-ajibu-hotuba-ya-dr-slaa-leo.html
http://msabaha.blogspot.com/
http://msabaha.blogspot.com/
http://msabaha.blogspot.com/2015/09/mbatia-ajibu-hotuba-ya-dr-slaa-leo.html
true
6741126810271918050
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy