Arsenal walibomolewa na Bayern Munich kwa mara nyingine tena na kujikuta wakitolewa katika michuano ya Klabu Bingwa Ulaya katika ngaz...
Arsenal walibomolewa na Bayern Munich kwa mara nyingine tena na kujikuta wakitolewa katika michuano ya Klabu Bingwa Ulaya katika ngazi ya timu 16 kwa kuzabwa jumla ya magoli 10-2.
Mchezo ulibadilika baada ya Laurent Koschielny kumvuta Robert Lewandowski katika eneo la hatari na kusababisha penati, mapema kipindi cha pili. Koschienly pia alioneshwa kadi nyekundu baada ya mwamuzi kubadili mawazo kufuatia kumuonesha kadi ya manjano awali.
Baada ya hapo mafuriko yalianza, yakiongozwa na Arjen Robben, akifuatiwa na Douglas Costa na Arturo Vidal aliyefunga mabao mawili.
Real Madrid yatinga robo fainali
Katika mchezo mwingine wa ngazi ya timu 16, Sergio Ramos alipachika mabao mawili na kuipatia ushindi Real Madrid wa mabao 3-1 waliokuwa wakicheza ugenini dhidi ya Napoli.
COMMENTS