Manchester United imekubali kamuachia kiungo wake wa kati Bastian Schweinsteiger, ili apate kujiunga na Chicago Fire. Makubaliano ...
Manchester United imekubali kamuachia kiungo wake wa kati Bastian Schweinsteiger, ili apate kujiunga na Chicago Fire.
Makubaliano
kati ya vilabu hivyo yaliafikiwa siku ya Jumatatu, na sasa yuko kwenye
harakati za kufanyiwa uchunguzi wa kiafya na kupata visa.Nahodha huyo wa zamani wa kikosi cha Ujerumani mwenye umri wa miaka 32, ametia sahihi mkataba wa mwaka mmoja kwa mujibu wa gazeti la Tribune la Chicago.
"Nina huzuni kwa kuwaacha marafiki zangu wengi huko Manchester United, lakini ninatoa shukran kwa klabu yangu kwa kuniruhusu kuchukua jukumu hilo, Alisema Schweinsteiger.
Wiki ijayo alifanya mazoezi na timu ya vijana ya Machester United wakati wanajiandaa kwa mechi ya Europa League dhidi ya FC Rostov.
Schweinsteiger, ambaye alijunga na Manchester United ikiwa chini na ukufunzi wa Louis van Gaal mwaka 2015, alifanya mazoezi na kikosi cha wachezaji wasiozidi miaka 23 wakati Jose Mourinho alichukua usukani msimu uliopita.
COMMENTS