MANCHESTER CITY YAONGOZA LIGI KUU ENGLAND

MANCHESTER CITY YAONGOZA LIGI KUU ENGLAND

 29 Januari, 2014 - Saa 23:12 GMT Facebook Twitter Google+ Tuma kwa rafiki yako Chapisha Mshambulizi Sergio Aguero wa Man...

DOWNLOAD NEW AUDIO FROM YOUNG DEE HANDS UP
Download new Hit from PAPA WEMBA ft DIAMOND PLATNUMZ CHACUN POUR SOI
New Song Emoo Classic _ Tulia

 29 Januari, 2014 - Saa 23:12 GMT
Mshambulizi Sergio Aguero wa Man City
Klabu ya Manchester City imechupa hadi kileleni mwa ligi kuu ya soka nchini England baana ya kuonesha soka safi dhidi ya klabu ya Tottenham katika uga wa White Hart Lane.
Kikosi cha kocha Manuel Pellegrini kilihitaji ushindi dhidi ya Spurs ili kuwapiku Arsenal kwenye jedwali la msimamo wa ligi hiyo, na matumaini hayo yalianza kuonekana mapema wakati Aguero alipovuna bao la kwanza, hii ikiwa ni mara ya nane mfululizo akiifungia City katika mechi nane mfululizo.
Yaya Toure aliiweka Man City kifua mbele kwa bao la pili, dakika ya tano kipindi cha pili kupitia mkwaju wa penalti uliozua utata ambapo mlinda ngome wa Spurs Danny Rose alitimuliwa uwanja kwa kulishwa kadi nyekundu japo alionekana kuugusa mpira kwanza kabla ya kuadhibiwa kwa kumchezea rafu Edin Dzeko.
Dzeko aliongeza bao la tatu na ingawa Etienne Capoue alifunga bao la kufuta machozi kwa Spurs, bado kulikuwa na fursa kubwa kwa Man City kuendelea kuinyeshea Spurs mvua ya magoli kupitia mchezaji wa akiba Stevan Jovetic aliyefunga bao lake la kwanza katika ligi kuu tangu uhamisho wake wa pauni £22m kutoka klabu ya Fiorentina ya Italia.
Aguero afunga mabao 50
Baada ya mechi hiyo Sergio Aguero sasa ameandikisha rekodi ya kufunga takriban mabao 50 ya ligi kuu baada ya mechi 81, na kuibuka kuwa mtu wa tano kufunga kiasi hicho cha mabao, baada ya Andy Cole, Alan Shearer, Ruud van Nistelrooy na Fernando Torres.
Kisha City ikaongeza maumivu zaidi kwa Spurs baada ya kile kipigo cha mabao 6-0 mwezi November mwaka uliopita, pale Vincent Kompany alipokamilisha kibarua kwa kufunga bao la tano na la ushindi.
Chelsea 0 - 0 West Ham
Kwenye matokeo ya mechi nyinginezo Chelsea ilipata pigo kwenye harakati zake za kutafuta uongozi kwenye jedwali baada ya kulazimika kutoka sare ya kutofungana na West Ham katika uwanja wa nyumbani Stamford Bridge.
Kwingineko Aston Villa iliishinda West Brom mabao 4 - 3 nayo Sunderland ikainyuka Stoke 1-0.
Hii ndiyo orodha ya saba bora tarehe 30-01-2014:
1 Man City 53
2 Arsenal 52
3 Chelsea 50
4 Liverpool 46
5 Tottenham 43
6 Everton 42
7 Man Utd 40
Name

AJIRA AND SCHOLARSHIPS,3,CELLEBS,5,love tips,1,MAGAZETI,5,michezo,8,MIX-NEWS,11,New audio,36,politics,1,sports,4,stori za mapenzi,1,technology,1,video,28,
ltr
item
MSABAHA BLOG: MANCHESTER CITY YAONGOZA LIGI KUU ENGLAND
MANCHESTER CITY YAONGOZA LIGI KUU ENGLAND
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2014/01/16/140116091114_sergio_aguero_512x288_reuters_nocredit.jpg
MSABAHA BLOG
https://msabaha.blogspot.com/2014/02/manchester-city-yaongoza-ligi-kuu.html
https://msabaha.blogspot.com/
http://msabaha.blogspot.com/
http://msabaha.blogspot.com/2014/02/manchester-city-yaongoza-ligi-kuu.html
true
6741126810271918050
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy