UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM KUMI BORA VYUO VIKUU VYA AFRICA

UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM KUMI BORA VYUO VIKUU VYA AFRICA

Z   Dar es Salaam. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kimeshika nafasi ya kumi miongoni mwa vyuo vikuu 50 bora na vyenye umaarufu Afri...

Z
 
Dar es Salaam. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kimeshika nafasi ya kumi miongoni mwa vyuo vikuu 50 bora na vyenye umaarufu Afrika.
Kadhalika UDSM kimetajwa kuwa miongoni mwa chuo vikuu chenye idadi kubwa ya wanafunzi na walimu na wingi wa programu za masomo.
Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala alisema chuo hicho kina haki ya kushika nafasi hiyo kutokana na jitihada zinazofanywa na uongozi.
“Tulifanya jitihada kuhakikisha tuna walimu wazuri wenye shahada za uzamili na uzamivu, maabara nzuri na miundombinu rafiki ya kufundishia,” alisema Mukandala.
Alisema UDSM ina mitaala bora inayoendana na wakati na inazalisha wataalamu wengi kwa mwaka.
“UDSM inachaguliwa na wanafunzi wengi na pia ina wanafunzi wa kimataifa,”alisema.
Katika matokeo ya utafiti huo uliofanywa na Taasisi ya Kimataifa ya Vyuo Vikuu na vya Kati (4ICU) ya Uingereza, chuo hicho kilishika nafasi ya 10 kati ya vyuo 50 vilivyopimwa kulingana na vigezo vya taasisi hiyo.
Hata hivyo, taasisi hiyo ilieleza kuwa hawapimi ubora wa vyuo kwa kuangalia kiwango cha elimu inayotolewa au huduma bali wanaangalia umaarufu wa chuo kimataifa.
“Huu mtandao si kwa ajili ya taaluma wala usichukuliwe kama kipimo cha kuchagua programu au nafasi ya masomo, huu ni kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wa kimataifa kufahamu jinsi taasisi ya elimu ilivyo maarufu katika nchi nyingine,” ilisema taarifa ya 4ICU.
Katika taarifa hiyo, Chuo Kikuu cha Cape Town cha Afrika Kusini kilishika nafasi ya kwanza huku vingine vilivyoshika tano bora vikitoka nchini humo.
Nafasi ya pili ilishikwa na Chuo Kikuu cha Pretoria, ya tatu Chuo Kikuu cha Stellenbosch na nne ilikwenda kwa Chuo Kikuu cha Witwatersand na tano ikishikwa na Chuo Kikuu cha Afrika Kusini.
Ikieleza namna walivyoweza kupata vyuo bora, tovuti ya 4ICU iliangalia jinsi mitandao mingine inavyozungumza na kutoa taarifa za chuo husika, nafasi yake katika kurasa za mtandao ya kijamii kutafuta taarifa kwa google, chuo kinavyotumiwa kama rejea katika taarifa mbalimbali na ni kwa kiasi gani watu wanaitumia tovuti ya chuo husika. chanzo

Name

AJIRA AND SCHOLARSHIPS,3,CELLEBS,5,love tips,1,MAGAZETI,5,michezo,8,MIX-NEWS,11,New audio,36,politics,1,sports,4,stori za mapenzi,1,technology,1,video,28,
ltr
item
MSABAHA BLOG: UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM KUMI BORA VYUO VIKUU VYA AFRICA
UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM KUMI BORA VYUO VIKUU VYA AFRICA
http://www.atlas-euro.org/Portals/0/Downloadables/Events/2015/udsm.JPG
MSABAHA BLOG
https://msabaha.blogspot.com/2015/04/university-of-dar-es-salaam-kumi-bora.html
https://msabaha.blogspot.com/
http://msabaha.blogspot.com/
http://msabaha.blogspot.com/2015/04/university-of-dar-es-salaam-kumi-bora.html
true
6741126810271918050
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy